Chuo Cha Simanjiro Cha Sayansi za Kilimo (SIAS), kilichopo Emboreet, Wilaya ya Simanjiro, kinatangaza udahili wa Mwaka wa Masomo 2026/2027 kwa Kozi ya Cheti cha Afya ya Mifugo na Uzalishaji (CAHP), NTA Level 4–5. Chuo kitafunguliwa rasmi tarehe 09/10/2026, na mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 15/08/2026. Wanaopenda kujiunga wanapaswa kuwa wamefaulu Kidato cha Nne au Sita, au kuwa na mafunzo ya ufundi (VETA) katika Afya ya Mifugo. Fomu za maombi zinapatikana katika Parokia zote za Jimbo Kuu Katoliki la Arusha. Kwa maelezo zaidi, wasiliana na SIAS kupitia simu +255 628 628 004 au barua pepe simanjirosias2025@gmail.com.



